/*Start Css Menu*/ .menu{ border:none; border:0px; margin:0px; padding:0px; font-family:verdana,geneva,arial,helvetica,sans-serif; font-size:14px; font-weight:bold; color:8e8e8e; } .menu ul{ background:url(http://3.bp.blogspot.com/-jEZvPu90bIA/TjlATeBIGoI/AAAAAAAAE4A/shxxdvs2fHI/s1600/menu-bg.gif) top left repeat-x; height:43px; list-style:none; margin:0; padding:0; } .menu li{ float:left; padding:0px 8px 0px 8px; } .menu li a{ color:#666666; display:block; font-weight:bold; line-height:43px; padding:0px 25px; text-align:center; text-decoration:none; } .menu li a:hover{ color:#000000; text-decoration:none; } .menu li ul{ background:#e0e0e0; border-left:2px solid #a80329; border-right:2px solid #a80329; border-bottom:2px solid #a80329; display:none; height:auto; filter:alpha(opacity=95); opacity:0.95; position:absolute; width:225px; z-index:200; /*top:1em; /*left:0;*/ } .menu li:hover ul{ display:block; } .menu li li { display:block; float:none; padding:0px; width:225px; } .menu li ul a{ display:block; font-size:12px; font-style:normal; padding:0px 10px 0px 15px; text-align:left; } .menu li ul a:hover{ background:#949494; color:#000000; opacity:1.0; filter:alpha(opacity=100); } .menu p{ clear:left; } .menu #current{ background:url(http://1.bp.blogspot.com/-NjNjSmAlq34/TjlATMvGF7I/AAAAAAAAE38/UxPs9Qg4Fyg/s1600/current-bg.gif) top left repeat-x; color:#ffffff; } /*End Css Menu from http://www.spiceupyourblog.com*/

Powered by Blogger.

Tuesday, February 19, 2013

MZEE KAMBI APATA ULAJI MNENE GHOLLYWOOD


Tanzanian talented actor Ramsey Hashim is in Ghana, It is said that he has been offered  a film role and he will appear with Ghananian A-list film stars who have also acted in many number of Nollywood films. We failed to know the actors he will star together although we spotted him with Van Vicker, John Dumelo and other actors. Great congratulations to the actor for his international project. Tutakuletea news zaidi ili ujue kinachoendelea kuhusu this project. endelea kusoma this blog

Wednesday, August 1, 2012

STERWAT HALL BYE BYE AZAM!!


Klabu ya Azam FC inapenda kutoa taarifa kuwa mkataba wake na kocha Stewart John Hall kutoka nchini uingereza ulisitishwa rasmi jana Tarehe 31/07/2012 kwa makubaliano ya pande zote mbili.

Klabu ya Azam FC inajivunia mafanikio ya kocha Stewart Hall, na inampongeza kwa kazi nzuri aliyoifanya katika muda wote aliofanya kazi kama kocha mkuu na mkurugenzi wa ufundi.


Chini ya Stewart Hall, Azam FC ilifanikiwa kutwaa ubingwa wa Mapinduzi Cup, Kushika nafasi ya pili katika ligi kuu, Mashindano ya Urafiki na Kombe la kagame. Haya ni mafaniko ambayo hayajawahi kufikiwa na makocha wote waliotangulia na ni mafaniko ya kihistoria katika klabu ya Azam FC.



Azam FC inamtakia kocha Stewart Hall kila la heri, na inatarajia kuwa ipo siku katika siku za usoni kocha Stewart atarudi tena kufanya kazi na Azam FC.


Stewart Hall anaacha changamoto kubwa sana kwa mrithi wake ambaye atatangazwa hapo baadaye lakini kizuri ni kuwa, mrithi wa Stewart Hall atakuwa ni mwalimu anayefuata mfumo ule ule wa uchezaji ulioachwa na Stewart Hall kwani hiyo ndiyo (Playing Philosophy ya Azam FC)


Kwa sasa timu itakuwa chini ya Vivek Nagul na Kally Ongala

Imetolewa na Utawala
Azam FC

OFFICIAL:MRISHO NGASSA SASA ATUA RASMI SIMBA!!

Hatimaye klabu ya Azam FC ya Tanzania imemuuza mshambuliaji wake Mrisho Khalfan Ngassa kwenda klabu ya Simba SC.

Azam ambao walimsaini Ngassa kwa ada iliyovunja rekodi ya uhamisho kwa wachezaji wanaocheza Bongo, Million 55, wamemuuza Ngassa kwa ada ya millioni 25 iliyolipwa cash na mabingwa wa Tanzania Simba.

Akizungumza na mtandao huu meneja wa Azam, Patrick Kahemele amesema kamati ya ufundi ya klabu pamoja na uongozi walikubalina kumuweka sokoni Mrisho Ngassa mara tu baada ya kumalizika kwa michuano ya Kagame Cup ambayo iliisha kwa Azam kushika nafasi ya pili nyuma ya Yanga.

"Klabu iliamua kumweka sokoni Ngassa mara tu baada ya michuano ya Kagame kumalizika, kwa kuwa mwenyewe alionesha nia ya kujiunga na klabu yake ya zamani Yanga, sisi tuliwapa kipaumbele Yanga, lakini pia Simba nayo ilionesha nia ya kumtaka. Tukafungua bid na kutangaza tunahitaji $50,000. Yanga baada ya kuwajulisha juu ya hili wakatuma ofa ya millioni 20, Simba nao wakatuma millioni 25. Ofa zote zilikuwa chini ya kiasi tulichohitaji lakini baada ya majadiliano ya viongozi wote wa Azam tukaona bora tumuuze tu, kwa bei ya millioni 25.

"Kwa kuwa Simba walikuwa wameshafikia viwango na sisi lengo letu lilikuwa ni kumuuza Yanga, asubuhi ya leo tukawatumia email Yanga tukiwaambia waboreshe ofa yao na tukawaambia bid ya Ngassa itafungwa saa saba mchana, lakini hadi muda huo unafika Yanga hawakuwa wametujibu chochote, kitendo ambacho tulikitafsiri hawana nia ya dhati ya kumsaini mchezaji huyo, kwa upande mwingine Simba walikuwa tayari wamefikia dau tulilolitaka hivyo tukafunga bid na kumuuza mchezaji huyo kwa Simba," alimaliza Patrick.

Tunaendelea kumtafuta Mrisho Ngassa na pale tutakapompata tutawaletea taarifa rasmi kuhusu alivyopokea taarifa za kuuzwa Simba.

By Aidan Charlie

ZITTO KABWE AZUNGUMZIA SHUTUMA ZA RUSHWA DHIDI YAKE!!

Ndugu Waandishi,
Nalazimika kukutana nanyi kutoa maelezo juu ya tuhuma zenye shinikizo la kisiasa zinazoelekezwa kwangu binafsi kwamba hata mimi nimeshiriki katika vitendo vya rushwa, kwa nafasi yangu kama Mwenyekiti wa Kamati ya Bunge ya Mashirika ya Umma. Taarifa hizo, kama kawaida ya uzushi mwingine wowote  zimesambazwa kimkakati na kwa kasi kubwa kiasi cha kuukanganya umma.
Nafahamu nabeba dhamana kubwa ya uongozi, taswira yangu ya uongozi daima imeakisi njozi na matumaini ya wananchi wa Kigoma Kaskazini, wananchi wanyonge na vijana kote nchini bila kujali itikadi zao za kisiasa, jinsia zao, makabila yao na rika zao. Hivyo, nawajibika kupitia kwenu kuwatoa hofu juu ya hisia potofu zinazopandikizwa kwao na wale wasiopenda kuona baadhi yetu tukiwaunganisha na kuwasemea watanzania wasio na sauti, dhidi ya vitendo vya hujuma na vyenye dhamira ovu kwa taifa.
Mkakati huo wa kuniunganisha na baadhi ya Waheshimiwa Wabunge wanaotuhumiwa kwa kupokea Rushwa unatekelezwa kwa njia zifuatazo:
  1.   Kumekuwa na kauli za watendaji wa serikali ambao wamekuwa wakizieneza na hususan kutoa taswira kwamba baadhi ya kauli zangu zinatokana na ushawishi wa rushwa;
  2.   Kuna taarifa ambazo zimeandikwa tena katika kurasa za mbele za baadhi ya vyombo vya habari  zikidai ’’Zitto kitanzini’’ ama ’’Zitto sawa na popo nundu’’  zikiashiria kwamba na mimi ni mla rushwa; na
  3.   Waandishi wa habari na jamii kwa ujumla wamefikia kuaminishwa habari hizi kiasi cha wengine kuuliza kwa nini Mhe. Zitto Kabwe hakutajwa katika orodha iliyotolewa na Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani.
Ndugu Waandishi,
Naomba kutoa ufafanuzi wa hicho kinachoelezwa kwamba nina ushiriki katika masuala ya rushwa hususan kwenye masuala yanayohusu sekta ya Nishati na Madini:-
  1. Mara baada ya bodi ya Wakurugenzi ya  Shirika la Usambazaji wa Umeme Tanzania (TANESCO) chini ya Uenyekiti wake Meja Jenerali Mstaafu Robert Mboma kutangaza kwamba imemsimamisha kazi Mkurugenzi Mkuu wa Shirika hilo, Nd. William Mhando ili kupisha uchunguzi wa baadhi ya vitendo/mwenendo wake, Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) ambayo mimi ni Mwenyekiti wake ilimuandikia Mhe. Spika kumuomba aridhie ili Kamati iweze kuwaita Bodi ya TANESCO, Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu ya Serikali  (CAG) na pia Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kujiridhisha na tuhuma zote zinazotajwa zinafanyiwa uchunguzi wa kina na hatua kuchukuliwa;
  2. Kamati ya POAC ninayoiongoza ilimuomba Mhe. Spika kuwaita wahusika tajwa kwa kuwa zilikuwapo tetesi kuwa kusimamishwa kazi kwa Mkurugenzi huyo siku chache kabla ya Bajeti ya Wizara ya Nishati na Madini kulikuwa na lengo la kufunika ’madudu’ makubwa zaidi kwa kulichagiza Bunge na tukio hilo dogo, mkakati ambao naona umefanikiwa sana. Isitoshe, Kamati kutaka kujiridhisha na hatua za Bodi ni sehemu ya msingi ya utekelezaji wa majukumu ya Kamati yaliyowekwa kwa mujibu wa Kanuni za Kudumu za Bunge na pia Shirika la TANESCO ni moja kati ya mashirika ambayo yanawajibika kwetu kwa hesabu zake na pia ufanisi wake kwa ujumla. Tumefanya hivyo pia katika mashirika mengine, hili la TANESCO sio tukio la kipekee;
  3. Kitendo hiki cha halali na kwa mujibu wa Kanuni kilichofanywa na Kamati yangu  kimetafsiriwa kwa makusudi na baadhi ya watu kwamba ni ishara ya kuwa sisi au zaidi kwamba mimi nina maslahi binafsi na TANESCO na hususan Mkurugenzi wake Injinia Mhando, ndio maana tumetaka maelezo ya Bodi. Ukweli kwamba Kamati ya POAC tumewaita pia Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Mahesabu (CAG) na Mamlaka ya Udhibiti wa Manunuzi ya Umma (PPRA) kwa jambo hilo hilo umefichwa kwa makusudi!
  4. Baada ya  tukio hilo, nikiwa hapa Dodoma, mwandishi wa habari wa gazeti moja alinifuata akiniambia kuwa wamekutana na Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake, Nd. Eliachim Maswi hapa hapa Bungeni na wamewaambia kuwa mimi nimepewa rushwa. Hakutaja nimepewa rushwa na nani, kiasi gani na wala kwa lengo gani!
  5. Nimejaribu kumtafuta kwa simu Mhe. Waziri Mhongo na Katibu Mkuu wake ili wanipe ufafanuzi juu ya mimi na Kamati ya POAC kuhusishwa na tuhuma hizi bila mafanikio, hali ambayo inaniondolea mashaka juu ya ushiriki wao katika kueneza au kuthibitisha uvumi huo. Najaribu sana kujizuia kutokuwa na mashaka na ushiriki wao huo ikizingatiwa uzito na taswira ya nafasi zao katika jamii, lakini wameshindwa kunidhihirishia tofauti.
Sasa naomba kutoa ufafanuzi rasmi kuhusu mlolongo wa matukio hayo tajwa ambayo yanatumiwa na baadhi ya wanasiasa kuonesha kwamba eti nimehusika na vitendo vya rushwa.
  1. Binafsi sijawahi kuwa na mawasiliano ya aina yeyote na uongozi wa TANESCO kushawishiwa juu ya hatua ambazo POAC ndio imezichukua za kutaka kujiridhisha juu ya utaratibu uliotumika. Ieleweke wazi kabisa kuwa, hakuna wakati wowote, popote ambapo mimi binafsi au Kamati yetu imekataa Mkurugenzi Mkuu wa TANESCO kuchunguzwa kwa tuhuma zozote. Ambacho tumesisitiza wakati wote ni ufuatwaji wa taratibu, kanuni na sheria, hili nitalisimamia iwe masika au kiangazi;
  1. Ni kwa sababu hiyo, na kwa kujiamini kabisa nimeunga mkono suala la tuhuma za rushwa zinazotajwa zichunguzwe na Kamati ya Haki, Maadili na  Madaraka  ya  Bunge kwa kina;
  1. Nimekwenda mbali zaidi kukiomba chama changu CHADEMA kifanye pia uchunguzi na tathmini yake kwa kina kujiridhisha na tuhuma hizo;
  1. Natumia fursa hii pia kuomba vyombo vya Dola vichunguze tuhuma hizo kwa nafasi yake ili kuweza kupata ukweli;
  1. Ninaahidi kushiriki kikamilifu iwapo nitatakiwa katika uchunguzi wowote utakaofanywa na niko tayari kuwajibika iwapo nitakutwa na hatia yeyote.
Napenda niwatoe hofu wananchi wa jimbo la Kigoma Kaskazini walionituma kuja kuwawakilisha hapa Bungeni na Watanzania wote kwa ujumla kwamba:-
  1. Mimi Zitto Zuberi Kabwe sina bei, sijawahi kuwa nayo na sitarajii kuwa nayo huko mbeleni. Daima nimesimamia kidete maadili ya uongozi bora katika maisha yangu yote ya siasa, na nawaahidi sitarudi nyuma katika mapambano dhidi ya rushwa katika nchi hii pamoja na mikakati ya aina hii ya kunidhoofisha na kunivunja moyo;
  1. Nafarijika na salam mbali mbali zinazotolewa kunifariji na kusisitiza kuwa nisilegeze kamba katika mapambano haya, nimepokea ujumbe mwingi kwa simu, sms, tweeter na hata facebook na niko pamoja nanyi Watanzania wenzangu kamwe sitarudi nyuma hadi kieleweke. Naamini katika nchi yetu tunazo rasilimali za kutosha mahitaji/haja ya kila mmoja wetu lakini si ‘tamaa/ulafi’ wa baadhi ya watanzania wenzetu;
  1. Napenda kuweka rekodi sawa kwa Watanzania kwamba nimekuwa Mbunge hiki ni kipindi cha pili, Mimi ni Mwenyekiti wa Kamati ya Hesabu za Mashirika ya Umma (POAC) huu ni takriban mwaka wa saba sasa, Kamati yangu inasimamia mashirika 259 ya Umma na si TANESCO peke yake. Mchango wa Kamati hii katika Bunge na kwa ustawi wa Mashirika ya Umma ni bayana na haujawahi kutiliwa shaka. Kamati yetu imeokoa upotevu mkubwa wa mali za umma na kuokoa fedha za umma kutokana na umakini wake. Tumefanya hivyo CHC hivi karibuni, Kiwira na kwenye mashirika mengine mengi. Kote huko uadilifu na uzalendo wa Kamati hii haujawahi kuhojiwa. Inatuwia vigumu kuona kuwa tunahojiwa katika suala hili la TANESCO. Hapa pana kitendawili.
  1. Zipo hoja pandikizi za kutaka Kamati ya POAC ivunjwe na haswa zikinilenga mimi binafsi. Nafahamu kiu ya wasioitakia mema nchi yetu kuiona POAC ikivunjwa au sura zikibadilishwa kwa kuwa Kamati hii imekuwa mwiba kwa mikakati yao ya kifisadi. Kwa maoni yangu, Kamati ya POAC isihusishwe na tuhuma hizi kwa vyovyote vile. Niko tayari nihukumiwe mimi kama mimi na sio kuhusisha wajumbe wengine ambao hawatajwi mahala popote katika tuhuma hizi mbaya sana katika historia ya Bunge letu. Nitakuwa tayari kunusuru Kamati ya POAC na maslahi ya taifa letu kwa kujiuzulu Uenyekiti iwapo itathibitika pasipo shaka kuwa nimehongwa. Kamati ya POAC ni muhimu zaidi kuliko mimi.
  1. Nafahamu pia kuwa kuna wanasiasa hasa wa Upinzani ambao wanautaka sana Uenyekiti wa POAC na wanafanya kila njia kutaka kuidhoofisha. Lakini hawajui kuwa anaepanga wajumbe wa Kamati ni Spika wa Bunge.
  1. Msishangae pia kuja baadae kubaini kwamba baadhi ya wanasiasa wenye midomo mikubwa ya kutuhumu wenzao wao ndio vinara wa kupokea rushwa.
  1. Ni lazima tufike mahali kama viongozi kwamba utaratibu unapokiukwa na yeyote yule, au uongo unapotolewa hadharani tuseme bila kuogopa. Hili ndio jukumu letu kama wabunge na viongozi. Kusimamia ufuatiliaji wa utaratibu ni jukumu letu kama Kamati ya POAC na ndio sababu ya msingi ya kuanzishwa kwa mamlaka kama CAG na PPRA. Haiwezekani, tuwe na set ya kanuni kwa kundi fulani na nyingine kwa makundi mengine, au kuhukumu ufuataji wa taratibu kwa kuangalia sura ya mtu usoni
Mwisho
Kumejengeka tabia hivi sasa ya kuwamaliza wanasiasa wenye kudai uwajibikaji na uzalendo. Kumeanzishwa kiwanda kwenye medani ya siasa cha kuzalisha majungu na fitna zenye lengo la kuwachonganisha wanasiasa wa aina hiyo na wananchi kwa kutumia vyombo vya habari na nguvu ya fedha. Naamini mbinu hizi chafu, kama nyingine nyingi zilizojaribiwa kwangu huko nyuma nazo zitashindwa.
Naamini katika kweli na kweli daima huniweka huru. Naamini kuwa mwale mdogo wa mwanga wa mshumaa hufukuza kiza. Kwa imani hiyo, sitasalimu amri mbele ya dhamira zao ovu hata nitakapobaki peke yangu katika mapambano hayo ya kulinda na kutetea rasilimali za taifa zinufaishe watanzania wote.
Daima nitaongozwa na busara ya Hayati Shabaan Robert isemayo, ‘Msema kweli huchukiwa na marafiki zake, nitakapofikwa na ajali hiyo, sitaona wivu juu ya wale wawezao kudumu na marafiki zao siku zote, siwezi kuikana kweli kwa kuchelea upweke wa kitambo, nikajitenga na furaha ya kweli itakayotokea pale uwongo utakapojitenga”.
Ahsanteni sana

KWELI VODACOM KATIKA HILI WALIKOSEA!!

Awali ya yote napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza Vodacom kwa kuja na wazo zuri la kutambua michango na umuhimu wa mitandao ya kijamii, hususan blogs na web site na kuamua kuwatunuku.
Pamoja na pongezi hizo, lakini mmekosea katika utekelezaji wake. Kwa mtizamo wa  wahusika wengi (Blogers), tuzo mlizotoa baadhi zimeenda kwa wasiostahili na mmeacha wengi waliostahili kupata tuzo hizo.
Ingawa hamkuweka wazi vigezo vyote, lakini baadhi ya mlivyovitaja ni pamoja na blog kuwa inayofanyakazi (active), ambayo inaweka habari mpya kila siku, iwe inayoandika vitu halisi na siyo vya kukopi au kutafsiri kutoka BBC na mitandao mingine ya Kiingereza na kupesti.
Hali kadhalika mkasema kuwa web site au blog hiyo inachokiandika kiwe kimeandikwa na mtu mwenye ujuzi nacho, mkatoa na mfano kuwa kama ni mapishi, basi yaandikwe na mtu mwenye kujua mapishi. Pia mtandao huo uwe maarufu.
Bila shaka kwenye ulimwengu wa mitandao, unaposema mtandao fulani ni maarufu, ina maana unatembelewa na visitors wengi kwa siku, mtandao hauwezi kuwa maarufu kisha ukawa na visitors 500 au 800 tu kwa siku.
Bloggers maarufu nchini wanajuana na wanahesabika, inakuwa kichekesho inapokuja kutangazwa blog fulani ndiyo maarufu wakati haijulikani hata miongoini mwa bloggers wenyewe, achilia mbali wasomaji wengine.

Hawa ndiyo washindi wenyewe:

  1. Mikocheni Report,
  2. Issa Michuzi
  3. Wanamuziki Tanzania.
  4. Kipanya.co.tz
  5. Vijana FM
  6. Millardayo.com
  7. Taste of Tanzania
  8. Jamii Forums
  9. Mambo Magazine
  10. DJ Fetty Blog
 
Kwa mtizamo wa wengi, katika orodha hiyo ya watu kumi, ni wanne tu ndiyo walistahili na waliobaki hawakustahili kabisa, kwa sababu licha ya kuwa hawajulikani sana, lakini pia huoni hata namna ambavyo Vodacom, kama kampuni, inaweza kunufaika nao iwapo mtaamua kujitangaza kupitia kwao.
Kuna Bloggers wameachwa ambao wao ku blog ndiyo maisha yao, wanalala, wanaamka, wanatembea, wanakula, wanakunywa, wanakaa wana blog tu. Wao na Blog, Blog na wao. Hakuna taarifa, breaking news au picha za matukio yote muhimu zinazowapita hapa nchini na hata katika kuripoti matukio ya promosheni ya Vodacom kwenye mitandao yao wako mstari wa mbele. Wengine kazi yao ni kukopi na kupesti kazi za wengine!
Pengine hatuyajui malengo ya Vodacom, kwa sababu kama kweli mnanataka kuthamini michango ya 'social media' na wao kunufaika na media hizo, basi mmekosea katika hili.
Waulizeni mliowatuma, wamefanya research ya kutosha na kuona hao washindi wana visitors wangapi na pageviews ngapi kwa siku? Je, Google Analytics Report zao zinaoneshaje? Na, je, habari na picha wanazoziweka kwenye mitandao yao, kweli ni za kwao, au wamekopi na kupesti tu kutoka kwingine?
Naomba mliopewa kazi ya kuandaa tuzo hizi myachukue haya kama changamoto na kuyafanyia kazi ili msiharibu kazi nzuri inayofanywa na Vodacom nchini Tanzania na wala hatuyasemi haya kwa sababu  ya chuki binafsi, bali kwa ukweli na uwazi tu!

Wassalaam!
Global Publisherstz.com

EPIQ BONGO STAR SEARCH,DAR ES SALAAM NI BALAA,MAELFU WAFURIKA KUSHIRIKI!!

                                                   Warembo kama hawa nao wapo!!
                                         Umati wa washiriki wakiwa kwenye foleni
             Kadri muda ulivyosonga ndio foleni ilizidi kuwa kubwa na kufanya eneo kuwa dogo
                    Lazma upendeze bhana..wachezea million hamsini wewe!!
                           Pozi nalo muhimu.....msaani pozi bhana..au sio
                                 umati wa washiriki wakiwa kwenye foleni
         Sidhani kama kuna kabila limekosekana leo hapa coco beach kwenye usahili.....